Monday, December 24, 2012

KATIBA YA MISRI YAPITISHWA



 Katiba mpya wa Misri iliyoandikwa na bunge linalodhibitiwa na Waislamu imepitishwa kwa asilimia 64 katika duru ya pili ya kura ya maoni.
Afisa mmoja wa chama cha Udugu wa kiislamu amefahamisha kuwa katiba mpya ya Misri imepitishwa na wapiga  kura wa nchi hiyo baada ya kufanyika duru ya pili ya kura ya maoni. Afisa huyo ameyakariri matokeo ya kura ambayo siyo rasmi ya chama chake.
Katika duru ya pili ya kupiga kura iliyofanyika hapo jana watu wa Misri waliipitisha katiba mpya kwa asilimia 64. Katika duru ya kwanza asilimia 57 ya washiriki walipiga kura ya ndio. Afisa huyo aliekuwamo katika chumba kilichofuatilia upigaji kura, aliliambia shirika la habari la Reuters kuwa kwa mujibu wa hesabu za chama chake matokeo kamili ya duru ya pili ni asilimia 71 ya kura za ndio.
Timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars imeilaza timu ya taifa ya Zambia, Chipolopolo kwa bao moja kwa bila katika mechi ya kirafiki ya kimataifa iliyochezwa katika uwanja wa taifa mjini Dar es Salaam, Tanzania.
Katika mechi hiyo bao pekee la washindi, lilipatikana sekunde chache kabla ya kumalizika kipindi cha kwanza likitiwa kimiani na mshambuliaji Mrisho Ngassa.

No comments:

Post a Comment