Saturday, December 29, 2012

MWILI WA MWANAMKE ALIYEBAKWA WARUDISHWA INDIA

Mwili wa mwanamke wa India ambaye amefariki hospitalini nchini Singapore baada ya kubakwa kinyama mjini New Delhi utarejeshwa kwa ndege maalum ya kukodi baadaye leo Jumamosi(29.12.2012).
Balozi  wa  India  nchini  Singapore T.C.A Raghavan  amewaambia waandishi  habari, saa  kadha  baada  ya  mwanamke  huko  kufariki kutokana  na  viungo  vyake  kushindwa  kufanya  kazi  katika hospitali  nchini  Singapore  ambako  alikuwa  akipatiwa  matibabu.
Mwanamke  huyo  na  ndugu  wa  marehemu  watasafirishwa kwenda  India   katika  ndege  maalum  ya  kukodi  baadaye  mchana wa  leo  Jumamosi, (29.12.2012) , amesema  Raghavan.

No comments:

Post a Comment